February 10, 2016

Wavuvi na watendaji wa ghuba ya menai wilaya ya kusini kuzifuata sheria na taratibu za uvuvi zilizowekwa ili kuepukana na mizozo isiyo ya lazima inayojitokeza mara kwa mara.
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa idara ya maendeleo ya uvuvi Zanzibar Mussa Aboud Jumbe huko Makunduchi wakati akizungumza katika kikao cha kujadili mbinu za udhibiti wa uvuvi haramu unaoendelea kwa kasi katika vijiji mbalimbali vya kanda za pwani wilayani ya kusini.
Eneo hilo limekuwa likikumbwa na mizozo ya mara kwa mara hasa kati  ya wavuvi wa kijiji cha mtende na kizimkazi wanaolalamikiwa kuchukuwa wageni kutoka tanzania bara na maeneo jirani kuvua katika maeneo ya ukanda wao wa bahari.
Wavuvi hao wanadaiwa kutumia zana zisizoruhusiwa ikiwemo mabomu na chupa za gesi hali inayowatia hofu wananchi ya  kupungua kwa mazalio ya samaki na uharibifu mkubwa wa mazingira ya bahari.
Mkurugenzi mussa amesisitiza haja ya wavuvi na watendaji wa ghuba ya menai kuziheshimu na kuzitekeleza vyema sheria zilizopo ili kuhakikisha vitendo hivyo vinapungua kwenye maeneo hayo.
hata hivyo amesema serekali kwa kushirikiana na idara yake inaendelea na jitihada za kutafuta njia za kupambana na uvuvi haramu ili kuhakikisha rasilimali zilizopo za bahari zinatunzwa na zinaendelea kuwanufaisha wanavijiji wenyewe.
Nae Mkuu wa wilaya ya kusini Khamis Jabir Makame amesema serekali haitasita kuwachukulia hatua za kisheria wavuvi au watendaji wa ghuba ya menai watakaobainika kuenda kinyume na utaratibu.

Kikao hicho kimewashirikisha masheha, wavuvi, wakuu wa madiko, wenyeviti na makatibu wa kamati za uvuvi vijijini, pamoja na watendaji mbalimbali wa ghuba za Menai.

0 comments:

Post a Comment