September 07, 2016

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa Msumbiji na Tanzania ni nchi zenye historia katika uhusiano na ushirikiano wao hivyo kuna haja ya kuendelezwa na kuimarishwa zaidi kwa manufaa ya pande mbili hizo.
Dk. Shein aliyasema hayo leo wakati wa mazungumzo kati yake na Balozi mpya  wa Msumbiji katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniam Monica Patricio Clemente Mussa  aliyefika Ikulu mjini Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha.
Katika mazungumzo hayo, Dk. Shein alisema kuwa uhusiano na ushirikiano kati ya Tanzania na Msumbuji ni wa kihistoria ambao umeasisiwa na viongozi wa wa Mataifa hayo akiwemo Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Marehemu Mzee Abeid Amani Karume na Hayati Samora Machel.
Akisisitiza juu ya uhusiano na ushirikiano wa kidugu kati ya Zanzibar na Masumbiji, Dk. Shein alisema kuwa katika kuliimarisha hilo Zanzibar hivi sasa kuna WanaMsumbujini wengi wanaoishi na waliozaliwa ambao wanaishi na Wazanzibari kama ndugu.
Kutokana na juhudi na hatua hizo, Dk. Shein alisema kuwa mashirikiano katika sekta kadhaa za maendeleo ni muhimu na ya msingi kwani yanaweza kuleta tija na mafanikio zaidi kwa pande zote.
Aidha, Dk. Shein alitumia fursa hiyo kutoa pongezi kwa mafanikio makubwa iliyoyapata Msumbiji katika kuimarisha uchumi wake sambamba na mafanikio katika sekta nyengine za maendeleo.
Aidha, Dk. Shein alisema kuwa Zanzibar ikiwa ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inathamini sana uhusiano na ushirikiano huo uliopo kati ya Msumbiji na Zanzibar na kueleza kuwa mashirikiano yanayoendelezwa yatasaidia katika uimarishwaji wa sekta za maendeleo zikiwemo elimu, kilimo, gesi na mafuta, biashara, utalii na nyenginezo.
Akizungumzia kwa upande wa sekta ya elimu, Dk. Shen alisema kuwa Zanzibar imeweza kupiga hatua katika sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na kuwa na Vyuo Vikuu Vitatu hivi sasa na kusisitiza haja kwa Msumbiji kuleta wanafunzi wake ili kuja kusoma Zanzibar ikiwa ni pamoja na kujifunza Lugha ya Kiswahili kupitia Chuo chake Kikuu cha Taifa cha SUZA.
Pia, Dk. Shein akitilia mkazo sula hilo alieleza kuwa hatua hiyo itasaidia katika kubadilishana uzoefu ambapo itawapa fursa na wanafunzi wa Zanzibar kwenda nchini humo kusoma lugha ya Kireno kwa lengo la kuiimarisha lugha hiyo hapa nchini ambayo ina historia kubwa katika historia ya Zanzibar na Utawala wa Kireno uliotawala hapa Zanzibar mnamo miaka ya 1500.
Dk. Shein alitumia fursa hiyo kumkaribisha Balozi huyo hapa nchini pamoja na kumpongeza Rais wa Nchi hiyo  Filipe Nyusi kwa mafanikio yaliopatikana ya kiuchumi na kimaendeleo.
Nae Balozi wa Msumbiji katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Monica Patricio Clemente Mussa, alisema kuwa Msumbiji inajivunia uhusiano na ushirikiano uliopo kati yake na Tanzania ikiwemo Zanzibar ambao ni wa muda mrefu.
Katika maelezoa yake Balozi huyo wa Msumbiji alisema kuwa  nchi hiyo hivi sasa imeqweza kupata mafanikio makubwa kwani tayari uchumi wake unazidi kuimarika siku hadi siku.
Aidha, Balozi Mussa alisema kuwa miongoni mwa sekta ambazo hivi sasa zinaimarika ni pamoja na sekta ya miundombinu, kilimo, madini, gesi na mafuta huku akisisitiza kuwa uchumi wa nchi hiyo inaendelea kukua na kuimarika.
Katika mazungumzo yao viongozi hao pia, waligusia haja ya kukuza uhusiano na ushirikiano katika sekta za  maendeleo.
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imeshauriwa kuanzisha mitaala itakayowafundisha wanafunzi mbinu za kujiepusha na vishawishi vya ngono vinavyoweza kuwaletea madhara na mbimba za umri mdogo.
Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) Fatma Iddi Ali, amesema mafunzo hayo ni muhimu ili kuwalinda watoto wa kike dhidi ya watu waovu.
Akiwasilisha mada kwenye warsha ya mafunzo kuhusu vitendo vya udhalilishaji ametaja madhara yatokanayo na mimba za umri mdogo ikiwemo vifo vya mama na watoto na kuharibika kwa mfumo wa uzazi.
Ameeleza kuwa kuathirika kwa kizazi husababisha mama kutolewa fuko la uzazi na hivyo kumfanya asiweze kubeba ujauzito kabisa.
Aidha amewakumbusha wazazi wajibu wa kukaa na kuzungumzana watoto ili waweze kufahamu matatizo waliyonayo na kutafuta njia za kuyatatua mapema.
Mjumbe huyo wa ZAFELA pia amesisitiza jukumu la wazazi na wanajamii kurejesha malezi ya asili na kushirikiana katika kuwalea watoto ili wakue katika maadili mazuri. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Saada Salum Issa, amewahimiza wazazi kujenga utamaduni wa kufuatilia maendeleo ya watoto wao maskulini, hasa katika masomo ya ziada (Tuitions) kwani baadhi yao huitumia fursa hiyo kujiingiza katika vitendo viovu.
“Pamoja na hayo, wazazi pia wanapaswa kutowadekeza mno watoto wao kwani  kufanya hivyo kutawapa kiburi na kuvuka mipaka ya nidhamu,” amesema.




"MAELEZO
Chuo cha Uongozi wa fedha Zanzibar (ZIFA) kiliandaa ziara ya siku moja ya mafunzo kwa wakulima wa mwani wa Chwaka kutembelea kikikundi cha Ushirika cha Tusife Moyo cha Kijiji cha Kidoti ambacho kimepiga hatua kubwa katika kusanifu zao hilo kwa ajili ya matumizi mbali mbali.
Ziara hiyo  ni moja ya juhudi zinazochukuliwa na chuo katika azma  yake ya  kusaidia jamii kufikia maendeleo  endelevu ya kiuchumi na ustawi wa jamii.
Mhadhiri wa ZIFA Maalim Said  Mohd Khamis alisema kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na chuo cha Uongozi wa Fedha Zanzibar mwaka jana, ulionyesha kuwa zao la mwani ambalo linawashirikisha asilimia 80 wananchi wanaoishi pembezoni mwa bahari, wengi wao wakiwa wananwake bado halijamsaidia  mkulima ipasavyo.
Alisema kutokana na kasoro hiyo  chuo kimeamua kutoa msukumo maalumu wa kutoa mafunzo ya vitendo  kwa wakulima wa mwani ili wawe na uwelewa wa kulisarifu zao hilo kwa matumizi mengine  badala ya kuwauzia wafanyabiashara  kwa  bei wanayopenda wao.
Maalim Said alisema wakulima wa mwani wanatumia muda na rasilimali nyingi katika  kushughulikia kilimo hicho huku tija wanayopata ni ndogo  na haikidhi nguvu wanazotumia.
Aliswashauri wakulima wa  mwani wa Chwaka kujikusanya  na kuanzisha vikundi vya ushirikia ili waweze kupatiwa mikopo na misaada ya kununulia mashine za kusarifu mwani kwa matumizi mengine kama wanavyofanya wakulima wenzao wa kijiji cha Kidoti badala ya kuuza bidhaa hiyo kwa bei ndogo.
Kikundi cha Tusife moyo cha Kidoti kinamiliki mashine ya kutengenezea sabuni na mashine ya kusagia mwani mkavu kwa matumizi mbali mbali ambapo kilo moja ya mwani uliosagwa inauzwa shilingi 10,000 na kabla ya kusaga wanauza  shilingi 300
Katibu wa kikundi cha Tusife moyo cha Kidoti Hawa Simai Khamis aliwaeleza wakulima wa mwani wa kijiji cha Chwaka kwamba mafanikio waliopata yanatokana na kujikusanya pamoja na kutafuta wafadhili wa ndani na nje ya nchi
Amesema wanauweza wa kuzalisha aina tofauti za sabuni na wamepata soko katika baadhi ya mahoteli  ya kitalii yaliopo ukanda wa  Nungwi, Matemwe na Pwani Mchangani.
Katibu huyo aliongeza kuwa mwani kwa sasa ni chakula na unatumika katika vyakula vingi ikiwemo mchuzi, keki , juisi, kachumbari  na pia unatumika kutibu maradhi mengi ikiwemo maradhi ya ngozi.
Wakulima wa mwani kutoka Chwaka walifundishwa kutengeneza sabuni na kupika mchuzi  wa kukaanga kwa kutumia zao hilo  na kujifunza matumizi mengine .
Wakulima wa Chwaka walikishukuru Chuo cha uongozi wa Fedha Zanzibar kwa kuwaandalia ziara hiyo na wameahidi kuyafanyia kazi mafunzo waliyopata ili kuwa mkombozi wao kupitia zao la mwani.
Aidha walikishauri Chuo hicho kuendelea kuwapatia mafunzo zaidi  na kuwasimamia na kuwaongoza katika kuanzisha ushirika wa mwani wa Chwaka.


August 24, 2016



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amekutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa kampuni ya ZANTEL ukiongozwa na Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Millicom Group, Mauricio Ramos, ikulu mjini Zanzibar
Katika mazungumzo hayo rais Shein ameeleza haja kwa kampuni ya ZANTEL  kupitia  kuimarisha utoaji huduma zake ili kupata mafanikio zaidi katika ushindani wa kibiashara.
Amesema iwapo kampuni hiyo itafanikiwa katika utoaji huduma zake ndani na nje ya nchi kutasaidia kuitangaza Zanzibar kimawasiliano na kuinua uchumi wa Taifa
Dr. Shein amesema serikali ya Zanzibar itaendeleza ushirikiano wake na kampuni hiyo ambyo serikali ina hisa zake.
Nae Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Millicom Group,  Mauricio Ramos, amesema kampuni hiyo itahakikisha ZANTEL inapata mafanikio zaidi kutokana na mikakati madhubuti iliyowekwa hasa katika kuimarisha miundombinu yake ili kutoa huduma za uhakika.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Bw,Mauricio Ramos,Mtendaji Mkuu wa kampuni ya "Millicom Group"akiwa na ujumbe wake walipofika Ikulu Mjini Unguja kwa mazungumzo leo (kushoto) Nd,Benoit Janin Mtendaji Mkuu wa Zanztel  23/08/2016.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia)
 akisalimiana na Bibi Rachel Samren Naibu Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Millicom Group
 pia Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Zanztel (katikati) Bw,Mauricio Ramos,Mtendaji Mkuu wa kampuni 
ya "Millicom Group"(wa pili kulia) na (kushoto) Nd,Benoit Janin Mtendaji Mkuu wa Zanztel  ujumbe huo ulifika Ikulu Mjini Unguja leo kwa mazungumzo na Rais leo 23/08/2016

Mkurungenzi Mtendaji wa Millicom Group Mauricio Ramos akifurahia zawadi aliyokabidhiwa na wanafanya kazi wa kampuni ya simu za mkononi ya Zantel Zanzibar baada ya kufanya ziara ya kutembelea ofisi za kampuni hiyo Zanzibar.

Mkurungenzi Mtendaji wa Millicom Group Mauricio Ramos akiwa kwenye ya pamoja na wanafanya kazi wa kampuni ya simu za mkononi ya Zantel Zanzibar baada ya kufanya ziara ya kutembelea ofisi za kampuni hiyo Zanzibar.