November 03, 2014

Naibu kadhi Mkuu wa Zanzibar
Sheikh  Hassan Othman Ngwali
Naibu kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh  Hassan Othman Ngwali amesema bado baadhi ya wananchi wa Zanzibar hawajathamani amani iliyopo katika jamii kitendo kinachohatarisha kuibuka kwa migogoro ya kijamii.
Amesema mbali na kuwepo mitizamo tofauti ya kidini amani ni suala muhimu na iwapo litavunjika kutakuwa na ugumu wa kuabudu na kuwepo kwa maendeleo.
Akifungua mafunzo ya vijana wa dini tofauti wa Zanzibar Naibu Kadhi amesema ili kuwepo hali hiyo ni lazima kuheshimiana na kuvumiliana mawazo, imani na haki ya kila mtu na kusaidia  kuepusha mizozo isiyo na lazima.
Nae mchungaji Stanley Nicholas Lichinga amewataka vijana kuwa mabalozi wazuri katika kujenga maridhiano pamoja na kuwa makini katika matumizi ya teknolojia kwa misingi ya kuheshimu dini na utamaduni.
Akitoa maelezo mratibu wa jukwaa la maridhiano ya dini Daniel Nygaard amesema viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kuwa na umoja katika kuzungumzia suala la amani katika mahubiri yao katika jamii.

0 comments:

Post a Comment