November 03, 2014


Naibu katibu Mkuu
 

Serikali imesema haipo tayari kuona karafuu ya Zanzibar  inapoteza hadhi na ubora wake kutokana na kuchafuliwa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu.
Kauli hiyo imetolewa baada ya kutolewa malalamiko juu ya kupunguzwa uzito na kuchanganywa na vitu visivyohitajika kwa karafuu zinazosafirishwa nje ya nchi.
Naibu katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Mali asili Zanzibar Juma Ali Juma akizungumza katika semina ya ubora wa zao hilo  huko Pemba  amesema   hatua zitachukuliwa kudhibiti hali hiyo na wanapaswa kusimamia ni wakaguzi na wapasishaji katika vituo vya manunuzi.
Amesema wizara hiyo itaweka utaratibu wa kuwabaini watendaji watakaofanya uzembe ama kula njama katika kutekeleza wajibu wao wa kazi.
Nae Mkurugenzi Mwendeshaji wa shirika la Biashara la Taifa Zanzibar ZSTC Mwanahija Almas Ali amesema wamefanikiwa kupata mashine ya kupima ubora wa karafuu kwa majaribio na iwapo itafanikiwa zitawekwa katika vituo vyote vya manunuzi.

0 comments:

Post a Comment