February 10, 2016

Kamisheni ya Utalii Zanzibar imeandaa mikakati mipya ya utalii na kuacha kutegemea zaidi nchi za Ulaya kwa kuandelea kujitangaza zaidi kiutalii katika masoko  mapya ya nje ya nchi ili serikali kukuza uchumi wake.
Amesema Kupanuka kwa soko hilo kutasaidia kuondokana na utegemezi wa soko la nchi za bara hilo ambazo zinakabiliwa na changamoto kadhaa hali iliyopunguza mchango wa kwa sekta ya utalii.
Akizungumza  na waandishi wa habari kuhusiana na kuanzishwa kwa safari ya ndege ya Ukraine hapa Zanzibar, Naibu katibu mkuu wa wizara hiyo Issa Mlingoti amezitaja baadhi ya nchi ziliomo katika masoko hayo mpya yanayochipukia na wamepanga kuyafikia kikamilifu ni china, india, Israel, urusi na Ukraine
Amebainisha kuwa takwimu za uingiaji watalii kutoka nchi hizo ndani ya kpindi cha miaka iwili 2014 -2015 imwapa moyo na nguvu inayohitajika ni kasi ya kujitangaza zaidi
‘Israeli wageni wake wanatembelea Zanzibar wamefikia 7546 kutoka 3818 na , wageni kutoka Poland wameongezeka kutoka 3163 hadi 4083 katika kipindi hicho chs miaka miwili’, amsema Mlingoti.
Amefahamisha kuwa katika mpango huo wa kujitangaza zaidi Febuari 12 ndege ya kwanza inatarajiwa kuingia Zanzibar moja kwa moja kutoka Ukraine itashusha watalii 250 ambao watakaa Zanzibar kwa kiindi cha siku tisa.
Naibu Mlingoti ameeleza kuwa ndege hiyo imedhaminiwa na na kuletwa na kampuni ya Traveling Profession Group kutoka Ukraine kwa kushirikiana na  Sun Tours and Travel Zanzibar.

Amesema wanategemea ndege hiyo itafanya safari zake hizo za Zanzibar mwaka mzima kama kutakuwa na mafaniko zaidi.

0 comments:

Post a Comment