Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza kufuta posho za Wabunge wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania za vikao vya kamati zao za kisekta ili kupunguza matumizi
yasiyokuwa na lazima.
Huo ni miongoni mwa mipango yake ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili fedha
zitumike kuimarisha huduma za jamii.
Akitangaza uamuzi huo jana Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru amesema
kuwalipa posho ya vikao vya bodi ni kufanya malipo mara mbili kwa kazi moja wakati
vikao hivyo ni sehemu yao ya kazi.
Pia vikao vya bodi za mashirika ya umma vimepunguzwa hadi
kufikia vikao vinne tu kwa mwaka.
Msajili Mafuru alitoa agizo hilo katika mkutano na wakuu wa
taasisi na mashirika ya umma na pia wenyeviti wa bodi zao na kueleza kuwa
limetolewa na Rais Magufuli na kinachotakiwa ni utekelezaji wake.
0 comments:
Post a Comment