December 01, 2015

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya ukimwi Duniani  Tume ya UKIMWI Zanzibar ZAC imeandaa mkakati wa tatu wa kitaifa wa kumaliza maambukizi ya UKIMWI ifikapo 2030.
Mkakati huo utakwenda sambamba na utekelezaji wa programu maalum kwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ili  kujitambua kwa asilimi 90 ifikapo 2020.
Mkurugenzi Mtendaji wa ZAC Dk Ali  Salim Ali ametoa taarifa hiyo maalum ya Serikali katika kuadhimisha siku ya UKIMWI inayoadhimishwa kila ifikapo Disemba 1 na kwa mwaka huu ikiwa na kauli mbiu “Tumia fursa zilizopo katika kumaliza UKIMWI duniani”.
Akizungumzia kuhusu hali ya maradhi hayo Zanzibar amesema tafiti zinaonesha kuwa wanawake wanaojiuza miili yao na watumiaji wa  dawa za kulevya ndio wanaongoza kwa mambukizi kwa asilimia 10 kuliko kundi makundi mengine ya kijamii  zanzibar.
Dkt Ali ameongeza kuwa  utafiti huo uliofanyika kupitia mpango wa muda mfupi wa ZAC wa  mwaka 2007 na 2012 pia umebaini karibu watu 4000 wanajiuza na wengine kiasi ya watu 3000 wanajidunga sindano na wanaofanya mapenzi ya jinsia moja na wengine ni vijana wa umri kati ya miaka 15 hadi 16 Zanzibar.
Amesema kupitia mpango huo kumekuwa na mafanikio katika upimaji wa hiari wa mama na mtoto mbapo kwa sasa Zanzibar  ina vituo 156 ikilinganishwa na vituo 137 vya mwaka 2012 vinavyotoa huduma za ushauri nasaha na upimaji na upimaji wa hiari kwa mama wajawazito.

Hata hivyo  Mkurugenzi Ali amesema bado  UKIMWI  ni tishio duniani ikiwemo Zanzibar hivyo juhudi zinapaswa kuchukuliwa ili kufikia matarajio ya kuijenga Zanzibar bila ya UKIMWI.

0 comments:

Post a Comment