December 09, 2015


Jumla ya kesi 31 za makosa ya jinai yaliyofanywa na watoto zimewasilishwa katika mahakama mbalimbali za mkoa wa Mjini Magharib kwa kipindi cha miezi mitatu iliyopita.
Kati ya kesi hizo kesi 2 zimepatiwa dhamana, kesi 1 imekutwa na hatia na kesi 7 zimefutwa kutokana na kukosekana ushahidi.
Taarifa ya utekelezaji wa mradi wa marekebisho ya tabia kwa watoto wanaovunja  na walio katika hatari ya kuvunja sheria Zanzibar inaonesha tatizo la makosa ya jinai kwa watoto ni kubwa katika Mkoa wa mjini Magharibi ikilinganisha na mikoa mengine.
Mradi huo wa mwaka mmoja na nusu umefadhiliwa na shirika la kimataifa la UNICEF na kutekelezwa na taasisi  Kituo cha huduma za sheria Zanzibar Z.L.S.C na tanzania youth icon TAYI chini ya usimamizi wa idara ya ustawi wa jamii Zanzibar.
Akitoa taarifa hiyo mratibu wa mradi Abdallah Ahmed Sleiman kutoka kituo cha huduma za sheria Zanzibar amesema wanawasaidia watoto huduma za kisheria pamoja na kuwawakilisha watoto mahakamani.
Afisa kitengo cha ustawi wa jamii Nyezuma Said Issa amewataka watekelezaji wa mradi huo kuongeza juhudi za utoaji wa elimu, kutumia vyema rasilimali ili kupunguza tatizo hilo.
Nayo kamati ya hifadhi ya mtoto ya Wilaya ya mjini imeomba kuendelezwa ushirikiano  wa wadau katika ngazi zote ndani ya wilaya na kuwa karibu na familia kwa kuwa ni njia pekee ya kubaini vyanzo na sababu zinazowafanya watoto kufanya makosa.

0 comments:

Post a Comment