December 30, 2015

Wizara ya Ardhi Makaazi Maji na Nishati imetia saini kazi ya ujenzi wa mradi wa maji na usafi wa mazingira katika mji wa Zanzibar utakaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 34 zilizotolewa mkopo na benki ya Maendeleo Afrika ADB.
Utaiji wa saini wa utekelezaji wa mradi huo umefanyika kati ya mamlaka ya maji Zanzibar ZAWA na kampuni ya ujenzi kutoka  Iran kwa kushirkiana na kampuni ya Spencon Service limited ya Tanzania ambapo serikali ya Zanzibar itachangia asilimia kumi tu  ya fedha hizo.
Kwa mujibu wa makubaliano hayo mradi huo unatarajia kaunza hivi karibuni utahusisha ujenzi wa matangi ya maji katika maeneo ya Saateni na Mnara wa mbao, uchimbaji wa visima 10 vipya, kukarabati visima 20 vya zamani na kulaza kilomita 68 mabomba ya kusambazia maji
Akizungumza katika hafla ya utaiji saini Mkurugenzi mkuu wa ZAWA Dk Mustapha Ali Garu amesema lengo kuu ni kuhakikisha usambazaji wa huduma ya maji inafikia wananchi kwa asilimia 90 katika mji wa Zanzibar.
Waziri wa ardhi na makaazi Ramadhan Abdalla Shaaban amesema  serikali kwa sasa inakusudia kutafuta vyanzo mbadala vya usambazaji wa maji safi na salama ili kukabiliana na upungufu wa huduma hiyo Zanzibar. 

Hivyo mradi huo wa usambazaji wa maji katika mji wa Zanzibar ni kuhakikisha inafikia lengo hilo kikamilifu na kuondosha usumbufu wa kuoatikana huduma hiyo kikamilifu.   

0 comments:

Post a Comment