January 04, 2016

Tishio la ajira za Wafanyakazi 350 wa Kiwanda cha Sukari Mahonda zinaendelea kuwa hatarini kufuatia kuendelea kwa hujuma za kuyachoma moto mashamba ya miwa ya kiwanda sukari cha Mahonda Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Hii ni kufuatia Kiasi ya Eka 50 za Miwa iliyopevuka kuteketezwa kwa moto na  kusababishia Kiwanda hicho hasara ya Tani 200 za Sukari na Lita 2,300 za Spititi zilizogharimu zaidi ya shilingi Milioni 494 za Kitanzania.
Heka hizo zimechomwa na watu wasiojulikana ikiwa ni siku tano tangu baada ya  shamba hilo la Miwa kuchomwa karbu heka 150 Tarehe 30 mwezi uliopita.
Kwa mujibu wa  Kiwanda cha Sukari Mahonda  hasara iliyopatikana kwa  kiasi Eka 200 zilichomwa moto ni shilingi za Kitanzania  Bilioni 2,326,818,500/-.
Meneja wa Mradi wa Kiwanda cha Sukari Mahonda  Tushar Mehta amesema  kuendelea kwa hujuma hizo Uongozi wa Kiwanda hicho kinaweza kufikiria kufuta ajira mpya 450 za Wafanyakazi  baada ya kukamilika matengenezo makubwa na kuanza tena uzalishaji wa sukari.
Amemueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyefika kuangalia hasara ya moto uliotiwa katika shamba hilo katika kipindi cha siku Tano baada ya tukio kama hilo la Tarehe 30 mwezi uliopita.
Akitoa pole Uongozi wa Kiwanda hicho Balozi Seif amesema hujuma hiyo ya makusudi haiitakii mema Zanzibar katika harakati zake za kustawisha uchumi wake na amewasihi watu wenye tabia hiyo kuacha kwani inawavunja moyo wawekezaji walioamua kuja kuwekeza miradi yao ya kiuchumi  Zanzibar kwa lengo la kuisaidia Serikali pamoja na Wananachi wake.
 “ Haya ni Mashamba ya Serikali yaliyotengwa maalum kwa shughuli za harakati za Viwanda. Hivyo ndoto za baadhi ya Watu kufikiria kwamba  hujuma zao zitazaa matunda kwa kufanya wanavyotaka zinapaswa ziachwe mara moja ”. amesema Balozi Seif.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliufahaisha Uongozi wa Kiwanda cha Sukari Mahonda kwamba Serikali Kuu inaangalia mpango utakaowezesha Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kusaidia ulinzi kwenye Mashamba hayo ili kulinda hujuma zinazoonekana kushamiri siku hadi siku.

Hilo ni tukio la sita la hujuma za moto kwenye mashamba ya Miwa ya Kiwanda cha Sukari Mahonda  tokea kianze tena uzalishaji wa sukari na Spiriti mapema mwaka uliopita wa 2015.


Meneja wa Mradi wa Kiwanda cha Sukari Mahonda
Tushar Mehta akimueleza Balozi Seif hasara iliyopatikana
kutokana na hujuma ya moto kwenye
mashamba ya Miwa la kiwanda cha 
Sukari Mahonda,

0 comments:

Post a Comment