April 29, 2014

Wananchama wa chama cha wafanyakazi wa huduma za Umma na Afya ZPHE   wameiomba  Chama  cha wafanyakazi Zanzibar ZATU kufuatilia juu ya baadhi ya wafanyakazi wa taasisi za umma kusita kuingiza nyongeza za mishahara iliyoidhinishwa na Serikali.
 Wamesema  nyongeza hizo zimeshaingizwa kwa karibu miezi sita sasa lakini wafanyakazi katika baadhi ya taasisi hawajaingiziwa nyongeza hiyo ya shilingi 25,000 hadi sasa  wakati wote ni  wafanyakazi wanaotumikia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Wakitoa michango yao katika mkutano wa kutoa taarifa ya sherehe za wafanyakazi May day wameiomba ZATUC kufuatilia  kasoro hiyo kwa vile kinaonesha kutokuwepo haki na usawa kwa watendaji hao wa sekt ya umma.
Kwa upande mwengine wafanyakazi hao wameomba kuangaliwa uwezekano wa kuongezwa kiinua mgongo kwa wafanyakazi wanaostahafu kama wanavyopatiwa wanasiasa ili nao waishi maisha mazuri baada ya kustahafu.
Nae katibu mkuu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi Zanzibar ZATUC Khamis Mwinyi amesema watafuatilia tatizo hilo ili kuona haki inatekelezwa.
Ameeleza kuwa maadhimisho ya May day mwaka huu yameanza kwa shughuli za upandaji wa miti katika maeneo ya maruhubi na zitaendelea kwa maonyesho ya taasisi mbali mbali yatakayofanyika  katika viwanja vya amani.

0 comments:

Post a Comment