January 05, 2016

Wizara ya afya imetakiwa kutoridhia kuwa kuwepo majengo na vifaa vya tiba kama ndio kigezo pekee cha mabadiliko ya sekta ya afya wakati hakuna watendeji wa kutosha.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein amesema mpango huo ni lazima uwende sambamba na kuimarisha huduma za afya, kufanya utafiti na kutoa mafunzo kwa wafanyakaziwa kutoa huduma bora kwa wananch.
Ameeleza hayo  katika  hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi kwa majengo ya wodi ya watoto na wodi ya kutoa huduma za mama na mtoto yaliyopo Mmanazi mmoja, ikiwa ni maadhimishio ya miaka 52 ya mapinduzi ya Zanzibar.
Ujenzi wa wodi ya mama na mtoto inatarajiwa kugharimu euro  milioni 9.9 itakayohusisha na vituo 19 vya afya  na kwa upande wa wodi ya watoto unatagharimu dola milioni moja nukta 6.7 za kimarekani ambapo Zanzibar imetoa nusu ya gharama ya mradi huo unategemewa kumalizika mwakani.
Katika mealezo yake Rais Shein amesema ujenzi wa majengo hayo ni moja ya hatua muhimu katika kutanua Hospitali ya Mnazi mmoja kuwa ya rufaa ili kupunguza usafirishaji wa wagonjwa nje ya nchi hasa ya magonjwa wa figo na saratani.
Ameishukuru Serekali ya Norway na Uholanzi kwa kuisaidia Zanzibar  kufanikisha mradi huo unaokwenda sambamba na sera ya Mapinduzi iliyo asisiwa tokea 1964.
Nao Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania Jaap Frederiks na wa  Norway Hanne Marie Kaarstad wamesema wanaamini kuwa mradi huo utaleta tija kwa wananchi wa Zanzibar kulingana na ongezeko la idadi ya watu.
Hata hivyo wamewapongeza wananchi kuwa wastahmilivu mbali na kuwepo changamoto za kisiasa ili wanaamini kuwa mzozo huo utaisha ili kufikia maamuzi yanayosthiki huku wakiahidi kuendelea kusaidia  Zanzibar katika mipango yake mbalimbali ya meaendeleo.
Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania Bw.Jaap Frederiks alipokuwa akitoa salamu
 zake mbele ya Rais wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi 
Dk.Ali Mohamed Shein   katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi
 Wodi ya Watoto na wodi ya mama na mtoto leo ikiwa ni shamra shamra 
ya miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar



0 comments:

Post a Comment