
Amesema suala la Dawa za
kulevya hivi sasa limekuwa janga la Dunia na limeathiri watu wengi hasa Vijana
hivyo udhibiti wa matumizi yake unahitaji maamuzi magumu ya Serikali pamoja na
ushirikiano wa Kitaifa, Kikanda na Dunia kwa ujumla.
ameeleza kuwa kwa sasa wakati umefika kwa wananchi kulazimika kutoa ushirikiano ili kusaidia kufanikisha azma ya Serikali ya kupambana na biashara na matumizi ya dawa za kulevya Nchini.
Balozi Seif amefahamisha
kuwa licha ya changamoto zilizopo za utekelezaji wa sheria na kanuni katika
kukabiliana na wimbi la uingizaji, uuzaji na matumizi ya dawa hizo Zanzibar lakini
Serikali imefanikiwa kuwakamata wahusika wa biashara hiyo kiasi 48 na Kilo 354.7
za dawa za kulevya zikiwemo bangi na heroin katika kipindi cha mwaka 2015.
Aongeza kuwa kati ya watuhimiwa hao baadhi wamefikishwa kwenye
vyombo vya sheria na wawili wawili walifutiwa makosa yao baada ya kukosekana
ushahidi, na mashtaka 18 yanaendelea kusikilizwa mahakamani na mengine 28
yaliyobakia yanaendelea na kufanyiwa uchunguzi.
Ameitaja moja ya kikwazo ni
suala la rushwa alilodai kwa kiasi kikubwa kinakwamisha mafanikio dhidi ya vita
vya dawa za kulevya licha ya juhudi kubwa inayochukuliwa na katika kupambana nayo
Zanzibar.
“Wananchi wako karibu na
maeneo yanayolimwa na kuzwa bangi, Polisi na uhamiaji wanayo nafasi kubwa ya
kuwatambua wanaoingiza na kuuza dawa za kulevya, Ofisi ya Mkurugenzi mashtaka
inayo wajibu wa kutayarisha hati zisizokuwa na kasoro na mahakama ina jukumu
la kuharakisha kutoa hukumu stahiki kwa mujibu wa sheria “. Amesema
Balozi Seif.
Amesema hayo alipokuwa
akiweka jiwe la msingi jenzi wa Kituo cha Tiba na marekebisho ya Tabia kwa
Vijana wanaoacha Dawa za kulevya huko Kidimni, Wilaya ya Kati Unaguja ikiwa ni
shamra shamra za maadhimisho ya sherehe za kutimia Miaka 52 ya Mapinduzi ya
Zanzibar.
Mapema katika akitoa taarifa ya ujenzi wa
Kituo hicho Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Dr.Omar
Dadi Shajak amesema ujenzi wa kituo hicho unagharimiwa na Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar kwa zaidi ya Shilingi Bilioni 4.2 hadi kukamilika kwake kitakuwa
na uwezo wa kuhudumia Vijana wapato 200 ambapo pamoja na mambo mengine kutakuwa
na mafunzo ya kazi za amali, michezo na huduma nyengine za kurekebisha tabia.
0 comments:
Post a Comment