December 04, 2015


Serikali imewaagiza maafisa  wa  afya nchini  kuhakikisha  kila kaya inakuwa  na choo bora  ikiwa ni hatua ya kuhakikisha  jamii inaupekana  na magonjwa  yanayotokana na uchafu  mazingira.
Mpango huo pia  unalenga kwenda sambamba  na   suala la usafi wa mazingira  kuwa endelevu  kama ilivyoagizwa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Donan Mmbando, wakati wa mkutano wake na  waandishi  wa habari  uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa  wizara hiyo.
Katibu Mkuu huyo alieambatana pamoja na baadhi ya viongozi wa Ofisi ya Makamu wa Rais na ya Waziri Mkuu kwa ajili ya kuzungumzia kuhusu usafi  wa mazingira  katika kuadhimisha siku ya  Uhuru ya  Desemba 9, mwaka 2015, ugonjwa wa kipindupindu na polio.
“Wakuu wa mikoa na wilaya wanatakiwa kutekeleza agizo hili kwa kujiwekea utaratibu wa kufanya usafi maeneo yao,” amesema Dkt. Mmbando.
Amesema ugonjwa wa kipindupindu pamoja na magonjwa mengine yanayohusiana na uchafu huenea kwa kasi kutokana na hali duni ya usafi katika maeneo tunayoishi.
Takwimu zinaonesha kuwa kati ya taka ngumu zinazozalishwa ni asilimia 50 tu huzolewa na kupelekwa dampo na kiasi cha taka kinachobaki huzagaa katika maeneo mbalimbali hasa kando kando ya barabara, katika maeneo ya kukusanyia taka (Collection points), chini ya madaraja na katika maeneo ya wazi na kubabisha miji kuonekana michafu. 
Pia  kiasi asilimia 34 ya kaya ndizo zenye  vyoo bora na asilimia 12% hazina vyoo kabisa hali inayohatarisha afya ya jamii na kusababisha kuenea kwa urahisi kwa magonjwa ya kuambukiza.
Dkt amewataka watendaji hao, kusimimia suala hilo kwa kuzingatia sheria za afya  zilizopo, huku akizitaka halimashauri na mamlaka kuweka sheria ndogo ndogo ili kutekeleza agizo hilo Rais kwa vitendo.
Akizungumzia shughuli za usafi katika siku hiyo ya Uhuru amesisitiza kuhamasishwa jamii kwa njia mbalimbali ili kujitokeza kwa wingi katika maeneo yao na sehemu za kazi au biashara, vyombo vya usafiri wa abiria na vituo vya wasafiri kwa kushirikisha wadau mbalimbali ikiwa juhudi za kupambana na kipindupindu.
Tayari Mikoa mingine 20 imeathirika na ugonjwa huo ulio ibuka kwa mara ya Agosti15, 2015 katika mkoa wa Dar es Salaam na takwimu zinaonesha watu 9,906 walipata ugonjwa  huu  na kati yao jumla ya watu 149 wafariki  dunia na wagonjwa wengine wamepata matibabu na kuruhusiwa kurudi nyumbani hadi tarehe 2 Desemba, 2015.




Magreth Kinabo- MAELEZO DSM

0 comments:

Post a Comment