November 16, 2015

Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Zanzibar imesema matumizi ya teknolojia ya kisiasa katika kuimarisha mfumo wa takwimu ni njia pekee itakayosaidia kuandaa sera na kupanga mipango bora ya maendeleo ya taifa.
Kufanya hivyo kutasaidia kuwa na mfumo wa pamoja wa upatikanaji wa taarifa zenye uhakika na kutoa viashiria mbalimbali vya kiuchumi na kijamii kwa maendeleo ya Zanzibar.
Kaimu Mkurugenzi wa idara ya huduma za Kitakwimu na kiufundi wa ofisi hiyo Ali Idrisa Shamte amewaambia waandishi wa habari katika hafla ya maadhimisho ya siku ya takwimu Afrika yenye kauli mbiu “Takwimu bora kwa maisha bora”.
Amesema kauli mbiu hiyo inatilia mkazo kwa wazalishaji wa takwimu kuzalisha takwimu bora na kwa wakati kulingana na vigezo na miongozo kutoka kwa afisi hiyo ya Serikali ya Zanzibar.
Kaimu Mkurugenzi  Shamte Amesema hatau hiyo itasaidia katika kuwa na taarifa sahihi za katika kuandaa sera na mipango yao mbalimbali kwa maendeleo ya taifa.

Amefahamisha kuwa ofisi hiyo inaendelea kutoa viashiria mbalimbali kutipia tafiti kwa ajili ya utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya Zanzibar ikiwemo Dira ya Maendeleo ya 2020, mkakati wa MKUZA na malengo ya Milenia ya mwaka  2015.

0 comments:

Post a Comment