April 23, 2014

Mamlaka ya vitambulisho vya Mtanzania NIDA imesema inakusudia kufungua Afisi za kudumu za usajili kila Wilaya za Unguja na Pemba.
Afisa Usajili wa NIDA Zanzibar Said Kassim Mohd amesema vituo hivyo vitakuwa na jukumu la waliokosa na walikuwa hawajfika umri baada ya kukamilika  zoezi linaloendelea katika maeneo mbalimbali.
Akizungumzia kazi za uandikishaji wa vitambulisho hivyo katika Wilaya ya Wete na Chake Chake Pemba amesema kazi hiyo inaendelea licha ya kuweko kwa changamoto ndogo ndogo katika vituo vya uwandikishaji.
Akizungumza na Wandishi wa Habari Said ameeleza kuwa baadhi ya wananchi wamekuwa wanakaidi maelekezo yanayotolewa hali inayoleta ugumu katika kazi hiyo.

0 comments:

Post a Comment