April 23, 2014

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameiagiza Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo kuchukua hatua za dharura kukabiliana na changamoto zinazolikabili Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC).
Amesema ni lazima kuwepo mipango hio ili liweze kuendesha shughuli zake kwa mafanikio na kukabiliana ushindani mkubwa wa kibiashara
Dkt Sheni Amesema serikali imeshatoa fedha nyingi kwa Shirika hilo hivyo hakuna sababu ya kushindwa kujiendesha kibiashara.
 Amefahamisha kuwa serikali imewekeza kwenye na matumizi ya teknologia ya kisasa ikiwemo mradi wa digital Network hivyo hakuna sababu ya kusuasua mpango huo.
Ameziagiza taasisi za Serikali kufanyakazi kwa uwazi katika kupanga na kugawana rasilimali fedha ili pia kufanikisha utekelezaji wa malengo yaliyowekwa.
 Amesema utaratibu  huo ni njia pekee itakayosaidia kufikia malengo yaliyopangwa na Wizara kwa ufanisi.
Rais wa Zanzibar ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na uongozi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo kwenye kikao cha kutathmini utekelezaji wa mpango kazi na bajeti ya Wizara hiyo katika kipindi cha miezi tisa  kuanzia Julai 2013.
 

0 comments:

Post a Comment