Jumla ya wagonjwa 1974 wameambukizwa maradhi ya kipindupindu
na kati yao 22 wamefariki dunia tangu kuzuka kwa ugonjwa huo Zanzibar mwezi wa Septemba mwaka 2015 na 31 wanaendelea kupatiwa matibabu hadi sasa .
Daktari dhamana kanda ya Unguja Dkt. Fadhil Mohammed
Abdallah amesema bado ugonjwa huo ni tatizo na ameomba juhudi zaidi kuchukuliwa
ili wananchi wawe na mwamko wa kuchukua tahadhari kuhusu kujikinga
na maradhi hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari katika semina ya waandishi wa
habari juu ya kipindupindu mjini Zanzibar daktari mkuu kanda ya Unguja Dkt Fadhil
Mohamed abdalla mwamko huo utaifanya zanzibar kuwa salama.
Dkt. Fadhil Amesema kipindupindu huambukizwa na maji
yaliyochanganyika na kinyesi cha binadamu ambapo kwa mujibu wa utafiti
uliofanywa unainesha asilimia kubwa ya maji yanayotumika Zanzibar yana vimelea
vinavyosababisha maradhi hayo.
Amezitaja tahadhari hizo ni pamoja na kuweka
mazingira safi, kufuata masharti ya afya, kuchemsha maji ya
kunywa ama kutumia maji yaliyotiwa dawa ya kuulia bektiria wanaosababisha
maradhi hayo.
Hivyo Dkt. Fadhil amewasisitiza wananchi kuacha tabia ya kula
ovyo njiani, kukosha matunda na mboga mboga kabla ya kula na kuchukua
tahadhari kubwa wakati wa kumshughulikia maiti ya maradhi ya kipindu pindu
kwani ni miongoni mwa njia za maambukizi ya maradhi hayo.
Aidha amewataka waandishi wa habari kutekeleza majuku yao katika
kutoa elimu kwa wananchi ili wafahamu zaidi dhidi ya kukabiliana na
maradhi hayo.
“Waandishi wa habari
mnao mchango mkubwa wa kutoa elimu kwa jamii katika kukabiliana na
maradhi ya kipindupindu hivyo tunategemea ushirikiano makubwa
kutoka kwenu,” amesisitiza Dkt. Fadhil
Akifungua mafunzo hayo Mkurugenzi Mtendaji Kamisheni ya kukabiliana
na Maafa Zanzibar Ali Juma Hamad amesema juhudi za pamoja
zinahitajika kwa mtu na taasisi katika
kukabiliana na kipindupindu kwani si jambo la kawaida kuwepo kwa muda mrefu.
Akiwasilisha mada ya majukumu ya vyombo vya Habari katika
kudhibiti miripuko ya maradhi ya kuambukiza, Mkurugenzi wa Idara ya Habari
Maelezo Zanzibar Rafii Haji Makame amesema vyombo hiyo vinajukumu
la lazima katika kusaidia umma kudhibiti vifo na athari nyengine za kiuchumi na
kijamii zinazosababishwa na miripuko ya maradhi .
Hivyo ametaka kuongezwa ushirikiano kati ya vyombo vya habari na
sekta ya afya ili kupata taarifa sahihi kwa wakati katika kufikisha ujumbe kwa
umma.
mapema mwakilishi wa shirika la Afya Dunuia (WHO) Andemichael Ghirmay
amesema maradhi ya kipindupindu ni rahisi sana kukabiliana nayo kuliko maradhi
mengine ya miripuko iwapo kutakuwa na mikakati ya pamoja kati ya taasisi mbali
mbali zinazoshughulikia mazingira na usafi wa mji.
Wakati huo huo Katibu wa Jumuiya ya maafisa wa afya Zanzibar
Ahmed Suleiman Saidi amewashauri wananchi wa shehia ya Shaurimoyo kubadili
tabia na kuweka mazingira wanayoishi katika hali ya usafi ili kujikinga
na kipindupindu.
Ametoa ushauri huo alipokuwa akizungumza na wananchi wa shehia
hiyo walipowatembelea kutoa taaluma juu ya maradhi hayo kutokana kuwa ni
miongozi kati ya shehia zilizoathirika na kipindupindu.
Washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza kwa makini Daktari
dhamana Kanda ya Unguja Dkt. Fadhili Mohamed alipokuwa
akielezea njia za kukabiliana na kipindupindu.
|
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Rafii Haji Mkame
akiwasilisha mada ya wajibu wa waandishi wa habari katika kukabiliana na
maradhi ya miripuko Zanzibar |
0 comments:
Post a Comment