Rais
wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Vietnam Mhe. Truong Tan Sang amewasili nchi leo
kwa ziara ya siku tatu nchini Tanzania.
Rais
Sang amewasili nchini jana majira ya saa mbili usiku na
kupokelewa na waziri mkuu majaliwa kasim majaliwa ambapo akiwa nchini pamoja na
masuala mengine, atasaini mkataba wa unaolenga kuchochea biashara kati ya
vietnam na tanzania na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli.
Hii
leo amekutana, na Rais Magufuli aliewataka watanzania kujifunza kutoka kwa
Vietnam namna walivyoweza kupambana na umaskini kwa muda mfupi.
ameyasema
hayo Ikulu baada ya kusaini mkataba wa kukuza uhusiano baina ya Tanzania na
Vietnam.
“Tanzania
tunatakiwa tujifunze mambo mengi kutoka kwa wenzetu Vietnam ambao walipata
uhuru mwaka 1945 wakaingia kwenye mapigano mpaka mwaka 1976.
Wakati
huo pato la muvietnam mmoja lilikuwa dola 100 lakini leo ni dola 2000 na
wamepunguza umaskini kwa asilimia 50 kuifanya nchi hiyo kuwa ya kipato cha
kati,” alisema Mhe. Rais
Mhe.
Rais Magufuli aliongezea kuwa, mwaka 1976 Vietnam ilichukua mbegu ya korosho
kutoka Tanzania na kwenda kulima kwao, zao hilo limekuwa likifanya vizuri kwa
nchi yao na wanaongoza kwa kulima korosho Duniani. Kwa upande wa Tanzania zao
hilo limekuwa likitelemka chini kila mwaka.
Vilevile,
Mhe Rais alisema kuwa Vietnam ni nchi inayoongoza kwa uzalishaji wa samaki
lakini Tanzania ambayo ina maziwa 21 pamoja na mito na bahari kila mahali
haijaweza kuifikia Vietnam kwa uzalishaji wa samaki hivyo lazima watanzania
tujifunze na tusiogope kujifunza ili Tanzania itoke mahali iliko.
Aidha
Mhe. Rais alisema ziara ya Vietnam imekuja wakati muafaka wa kujenga mahusiano
mazuri kwa watanzania na nchi ya Vietnam lakini hasa katika uchumi ili Tanzania
iweze kufanikiwa namna ambavyo wao wamefanikiwa.
Kwa
upande wake, Mhe. Rais Truong alimshukuru Rais Magufuli na watanzania kwa
mapokezi mazuri na ameahidi kuimarisha mahusiano ya nchi hizi mbili hasa
katika sekta ya kilimo, biashara, mawasiliano pamoja na uwekezaji.
Mhe.
Rais Truong Tan Sang ni Rais wa kwanza wa nchi ya Jamhuri ya Kisoshalisti ya
Vietnam kufanya ziara nchini Tanzania. Rais huyo ameambatana na mawaziri wanne
pamoja na wafanyabiashara wapatao 30.
Mahusiano
ya Tanzania na Vietnam yalijengwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere na Kiongozi wa Vietnam, Ho Chi Minh kuanzia mwaka 1960 na kupelekea
kuanzishwa rasmi kwa mahusiano ya kidiplomasia mwaka 1965.
0 comments:
Post a Comment