January 30, 2016

Shirika la nyumba Zanzibar limeandaa mpango wa kuwatoza ada ya usafi wananchi wanaoishi nyumba za maendeleo za Michenzani hasa katika kukarabati makaro yao ili kuepusha maradhi ya mripuko.
kwa sasa shughuli za usafi katika nyumba hizo zinategemea fedha kutoka Serikalini kitendo kinachokwamisha shughuli za usafi katika majengo hayo. 
Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Mohammed Hafidh Rajab amesema utaratibu huo utasaidia kuzuia kero ya kuziba kwa  makaro  katika maeneo hayo.
Amesema shirika la nyumba limeamuwa kufuata utaratibu unaotumika katika mji mkongwe ambao umefanikisha mji huo unakuwa katika hali ya usafi na kuwa ni kivutio kizuri kwa watalii wanaofika nchini.
Akizungumza kuhusu ubovu wa makaro katika nyumba  namba 5 michenzani amesema tatizo hilo linatarajiwa kurekebishwa hivi karibuni kutokana na upatikanaji wa zaidi ya shilingi milioni 20 kutoka mfuko wa serikali zitakazotumika kufanya marekebisho  katika nyumba za Michenzani..

0 comments:

Post a Comment