November 15, 2015

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi 
wa habari nje ya ukumbi wa NEC ,CCM Makao Makuu Dodoma 


Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imewateua makada watatu watakaowania kuchaguliwa kugombea nafasi ya uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la 11 kupitia chama hicho.

Walioteuliwa kugombea nafasi hiyo na Kamati Kuu iliyofanyika chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni pamoja na Naibu Spika aliyemaliza muda wake JOB NDUGAI, Dkt. TULIA ACKSON na ABDULAH MWINYI.
Wana-CCM hao watatu watapigiwa kura na Kikao cha Kamati ya Wabunge wote wa CCM kitakachofanyika kesho Novemba 16, 2015 saa nne asubuhi katika ofisi za Makao Makuu ya CCM Dodoma ilikuchagua jina moja kugombea nafasi hiyo katika Bunge la Jamhuri ya Muungano.
Kwa upande wa Naibu Spika wa Bunge, mchakato wa kuchukua fomu kwa wabunge wa CCM wanaoomba ridhaa kugombea nafasi hiyo utaanza kesho Novemba 16, 2015 na kukamilika Novemba 17, 2015 saa kumi kamili jioni.
Hadi jana nafasi ya Naibu Spika mwanachama mmoja tu ndiye aliyekuwa amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo ambaye ni Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan ‘Zungu,’ lakini kutokana na kasoro za kanuni atatakiwa kuchukua fomu upya. 
CCM blog

0 comments:

Post a Comment