Meli mpya ya Serikali
ya Zanzibar Mv Mapinduzi II imewasili bandari ya Zanzibar.
Meli hiyo imetengenezwa
Meli hiyo imetengenezwa Korea ya kusini kwa gharama ya dola za Kimarekeni
milioni 30.6.
Mv Mapinduzi II ina uwezo wa kupakia abiria wasiopunguwa
1,200 pamoja na tani 200 za mizigo itakuwa
ikifanya safari zake Pemba pamoja na Dar es-Salam.
Kufika
kwa meli hiyo kunaonekana kutapunguza tatizo la usafiri na inaelezewa kuwa
itaanza kazi zake hivi karibuni mara tu baada ya
kukamilika taratibu za uhakiki.
MV Mapinduzi II
ilitarajiwa kuwasili Zanzibar Julai
2015 ilikwama nchini Mauritus kufuatia kuwekewa kuzuizi na kampuni ya Leomthong ya Thailand iliyokuwa inaidai
Shirika la Biashara za Nje Zanzibar BIZANJE lililokuwa linaingiza vyakula na
bidhaa mbalimbali katika miaka ya 80.
0 comments:
Post a Comment