December 02, 2015

Jumla ya watu 82 wamegundulika kuambukizwa virusi vya Ukimwi kati ya watu 16,160 waliopima kwa hiari Pemba.
Takwimu hizo zimetolewa na Afisi ya programu ya kudhibiti Ukimwi Pemba ZACP zinaonesha watu hao wamegundulika kuanzia Januari hadi Septemba 2015 baada ya kupima katika shughuli mbalimbali za uhamasishaji juu ya Ukimwi.
Takwimu za jumla zinaonesha kuwa maambukizi ya ugonjwa huo Pemba  imefikia asilima 3 lakini kwa kuangalia makundi maalum inakisiwa kufikia zaidi ya asilimia 5.
Kundi la vijana ndio linaloonekana kuathirika zaidi na maambukizi mapya kutokana  na sababu mbalimbali ikiwemo vishawishi miongoni mwao na ngono zembe.
Suala la usiri pia limetajwa kuwa ni changamoto inayotatiza juhudi za taasisi na jamii katika kutoa elimu kuhusu Ukiwmi kwa makundi mbalimbali kisiwani humo.

Taarifa hii imetolewa na mratibu wa kitengo cha mradi huo wa ZACP.




"zanzibar leo 

0 comments:

Post a Comment