Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim
Seif Sharif Hamad, amezungumza na waandishi wa habari katika hospitali ya Hindu
Mandal jijini Dar es Salaam, na kusema kuwa hali ya afya yake inaendelea
vizuri.
Maalim Seif ametoa taarifa hiyo kufuatia
kuugua ghafla jana asubuhi na kukimbizwa katika hospitali hiyo, ambapo alilazwa
kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Daktari wa Maalim Seif aliyeambatana naye
akiwa Dar es Salaam Dkt Omar Mohd Suleiman amesema tatizo kubwa lililomkabili
kiongozi huyo ni machofu aliyokuwa nayo baada ya kutokea safarini nchini India
Ijumaa iliyopita.
Amesema alilazimika kulazwa hospitali hapo
ili kupata uangalizi wa karibu na kupumzika, na kwamba afya yake inaendelea
vizuri na anatarajiwa kutolewa hospitalini hapo leo jioni.
Maalim Seif aliugua ghafla jana asubuhi
akiwa safarini kuelekea Dar es Salaam, hali iliyopelekea kukimbizwa
hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam, mara baada ya kuwasili katika
uwanja wa ndege.
0 comments:
Post a Comment