March 13, 2016

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar  Balozi Seif  Iddi  amesema  mwananchi hasa vijana hawezi kuwa mzalendo kama hajajifunza  historia ya taifa lake.
Amefahamisha kuwa ni muda mrefu wasomi nchini wamekuwa wakipuuza kuisomesha historia ya Zanzibar kwa kuhofia kutokubalika kwa watu wa aina fulani.
Balozi Seif amesema hayo katika kongamano la umoja wa wanafunzi wa vyuo vikuu na taasisi ya elimu ya juu wa CCM  wa Wilaya ya Dimani na kuwataka wasomi wa chama hicho kupiga vita kasumba hizo kwani bila ya kuielewa historia hawatoweza kuwa wazalendo wa kweli.
Balozi Seif amefahamisha kuwa iwapo vijana watakubali kujifunza taarifa halisi zilizopita kuhusu Zanzibar  za kabla na baada ya Mapinduzi ya mwaka 1964 wanaweza kuwa wanasiasa wazuri wenye kuchanganua mambo kuhusu matukio tofauti.
Amewakumbusha vijana hao kuelewa matukio ya udhalilishaji yaliyoukumba uchaguzi uliopita kwa baadhi ya akina mama walilazimika kupewa talaka kwa sababu za itikadi za kisiasa.
Akizungumzia kuhusu uchaguzi wa marudio unaotarajiwa kufanyika jumapili ijayo amewatoa hofu wananchi wa Zanzibar  kuwa unatarajiwa  kuwa salama na kuwataka mwananchi kuitumia haki yao  ya kupiga kura   

Mapema mwenyekiti wa umoja wa wanafunzi wa vyuo vikuu wilaya ya Dimani Abdulaziz Saleh Khamis ameiomba Serikali za Tanzania kuhakikisha  amani inakuwepo ili wananchi  kuendelea na harakati zake za kimaisha za kila siku.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu na
Elimu ya juu wa Wilaya ya Dimani Abdulazizi  Saleh Khamis
akitoa taarifa ya Umoja huo

0 comments:

Post a Comment