February 11, 2016

Wizara ya Afya Zanzibar kupitia kitengo cha malaria inakusudia kugawa vyandarua vilivyotiwa dawa 500,000 kwa wananchi mbalimbali ili kujikinga na mbu wanaoambukiza malaria.
Afisa uhamasishaji kitengo cha malaria Jokha Salum Hemed amesema vyandarua hivyo vinatarajiwa kugaiwa kunzia Machi 1 mwaka huu mpango utakaohusisha shehia 82  za Unguja na pemba.
Amesema  lengo la utoaji wa vyandarua hivyo ni kujilinda na maradhi ya malaria nchini.
Amesema serikali imejidhatiti kuhakikisha inamaliza maradhi ya malaria ambayo yanawaathiri zaidi wajawaziti na watoto.
Amewataka masheha kuhakiksha wanorodhesha kaya zote ili kuhakikisha wanapatiwa vyandarua hivyo.

Amewasisitiza  wananchi kuendelea kuchukuwa hatua dhidi ya malaria ikiwemo kuweka safi mazingira yao pamoja na kufukia vidimbwi vya maji ili kuondoa uwezekano wa mazalia ya mbu.



:zanzibar leo

0 comments:

Post a Comment