February 11, 2016

Naibu Waziri wa mambo ya ndani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hamad Yussuf Masauni amelitaka jeshi la polisi Zanzibar  kujipanga vyema juu ya matukio ya uhalifu yanayojitokeza hasa katika kipindi hichi cha kuelekea uchaguzi wa marudio.
Amesema kumejitokeza matukio ya uhalifu ya uchomaji wa moto yanayohusishwa na itikadi za kisiasa katika sehemu mbalimbali hali inayosababisha hofu kwa   jamii na mali zao.
Akizungumza  na maafisa wa jeshi la polisi  katika ofisi ya makao makuu ya jeshi hilo Kilimani mjini Unguja Masauni amesema ni vyema jeshi la polisi likajipanga kukabiliana na matukio hayo ili kuhakikisha nchi inabaki kuwa na amani wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi.
Hata hivyo amelitaka jeshi la polisi kukamilisha ripoti juu ya mapungufu yaliyotokea wakati wa uchaguzi mkuu uliopita ili kurekebishwa katika uchaguzi wa marudio.
Nae  Kamishna wa jeshi la polisi Zanzibar Hamdani Omar Makame amesema jeshi hilo limejipanga vizuri katika kukabiliana na matukio yote ya uhalifu hasa katika kipindi cha uchaguzi wa marudio wa March 20-2016 na kuhakikisha amani inatawala wakati wote wa uchaguzi na baada ya uchaguzi huo.
Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame akizungumza
 kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani  Mhe. 
Masauni alipofanya ziara katika Jeshi hilo Zanzibar  kujionea 
Utendaji wake akiwa katika ziara ya kujitambulisha.

 

0 comments:

Post a Comment