Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeonya vikali
kwamba vyombo vya Dola havitakuwa tayari kuona Watu wachache wanatumia hila na vishawishi vya kutaka kuharibu uchaguzi wa marejeo
unaotarajiwa kufanyika tarehe 20 Mwezi ujao.
Onyo hilo amelitowa Makamu wa Pili wa Rais
wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakati akizungumza na Wanachama wa CCM na wananchi wa
Kijiji cha Kengeja mara baada ya kulikagua Tawi
la CCM la Kijiji hicho lililochomwa moto
na watu wasiojuilikana usiku wa kuamkia jumatano.
Balozi Seif amesema ametahadharisha kuwa fujo
zozote zitakazotokea kabla na baada ya uchaguzi huo wakukamatwa na kupelekewa kwenye vyombo
vya Dola pamoja na Kiongozi atakayehusika na kuandaa vurugu hizo.
Amewaonya watu walioandaliwa kujihusisha na vitendo
vya vurugu ikiwemo kufanya hujuma dhidi ya mali na vifaa vya Wananchi yakiwemo majengo ya
Kisiasa kuacha mara moja tabia hiyo itaayowasababishia
kutiwa na baadaye kuchukuliwa hatau za kisheria.
Balozi Seif amesema vitendo vya hujuma
vinavyoonekana kuibuka nyakati hizi ni vibaya kwa vile vinaathiri maisha ya jamii
kutokana na athari za hujuma hizo
kuharibu miradi ya wananchi kama mashamba, Majengo ya Skuli na yale ya Raia pamoja na huduma za Maji
safi na salama.
Amesema Vyombo vya Dola bado vinaendelea kufanya
uchunguzi wa kuwabaini
watu waliohusika na vitendo hivyo wakiwemo wale watu wanaoendeleza kauli za chuki, hujuma na na kutaka
kuleta vurugu hapa Nchini.
Balozi Seif amewahakikishia Wanachama na Wananchi
hao kuwa Serikali itajizatiti kuongeza ulinzi wa kutosha utakaoleta faraja kwa Umma hasa
katika kipindi cha mpito kuelekea kwenye
uchaguzi wa marudio wa mwezi ujao wa
machi.
Amesema uhuru wa Jamii utalindwa ili kumpa fursa kila Mwananchi kuitumia haki yake ya Kidemokrasia kumchagua Kiongozi anayestahiki amtumikie katika uchaguzi huo wa marejeo.
Amesema uhuru wa Jamii utalindwa ili kumpa fursa kila Mwananchi kuitumia haki yake ya Kidemokrasia kumchagua Kiongozi anayestahiki amtumikie katika uchaguzi huo wa marejeo.
Mapema Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Nd. Vuai
Ali Vuai amesema Wanachama wa CCM wanasubiri kupiga kura ya marejeo ifikapo Tarehe 20
mwezi ujao.
amewataka wanachama hao wa Chama cha
Mapinduzi kuzipa mgongo hila zilizozoeleka kufanywa na baadhi ya wanasiasa za
kudanganya wananchi hali ya kisiasa
inavyokwenda nchini na tayari zimeshafikia
ukingoni.
Amefahamisha kuwa CCM muda mwingi ilikuwa tayari
kuridhia kila kitu katika kuiona nchi inaendelea kubakia salama na hatimae kufikia suluhu
ya kuundwa kwa Serikali na Umoja wa Kitaifa
Zanzibar lakini upande mwengine wa
upinzani unashindwa kufahamika hasa unataka nini.
Amevitaka vyombo vya Dola kutosubiri kutokea maafa wakati
watu wanaoashiria matamshi ya shari wanaeleweka
katika maeneo mbali mbali Nchini.
Ameeleza kwamba vyombo hivyo vina wajibu na haki ya kuwadhibiti watu wenye tabia hiyo.
Ameeleza kwamba vyombo hivyo vina wajibu na haki ya kuwadhibiti watu wenye tabia hiyo.
Hadi sasa athari ya gharama zilizotokea kutokana
na janga hilo la moto ulioathiri baadhi ya sehemu za paa, mlango na Boriti katika Tawi hilo
la CCM Kengeja bado hazijafahamika.
0 comments:
Post a Comment