February 13, 2016

Rais Dk John Pombe Magufuli amelihutubia taifa kupitia wa Wazee wa Dar e salaam amesema serikali haitamvumilia mtu atakaehatarisha amani ya nchi pamoja na kuwatahadharisha viongozi na wananchi wengine kuhusu ubadhirifu wa mali ya umma.
Katika hotuba yake hiyo ameainisha changamoto kadhaa zinazolikabili taifa na mikakati inayochukuliwa na Serikali ya awamu ya tano kupambana nayo pamoja na kuwaahidi wananchi kuwatumikia na kukabili matatizo yao.
Akizungumza na wazee hao wa Dar es salaam katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini humo, Rais Dk John Pombe Magufuli amewahakikishia Watanzania kwamba Serikali ya awamu ya tano amezungumzia kuhusu hali ya kisiasa visiwani Zanzibar na kueleza ni vigumu yeye kuingilia maamuzi ya tume ya taifa uchaguzi Zanzibar ambayo ni huru.
“ Napenda kuheshimu sheria na ZEC ina uhuru wa kuamua mambo yake lakini kama kuna tafsiri mbaya, na  mahakamani zipo sasa unamwambia Magufuli aingilie nini….. Jukumu langu kama amiri jeshi mkuu ni kuhakikisha amani ya Zanzibar inaimarika, yeyote atakaeleta fyoko fyko ajue vyombo vya usalama vipo” amesema Rais magufuli.


ZAIDI HII HAPA HOTUBA KAMILI SIKILIZA 





0 comments:

Post a Comment