February 13, 2016

Kitengo cha ufuatiliaji nyendo za maradhi kimesema kuna uwezekano wa Zanzibar kuwa na ugonjwa wa zika kutokana na mbu wanaoambukiza ugonjwa huo wa aina ya AEDES AEGYPTI anapatikana visiwani humo.
Mkuu wa kitengo hicho Dkt Salma Masauni Yusuf amesema hadi sasa hakuna  mgonjwa alibainika kuambukizwa ugonjwa huo.
Amesema mbu huyo anaishi kwenye mazingira machafu kama mbu wa malaria na kwamba huuma zaidi nyakati za mchana tofauti na mbu wa malaria ambae anaumwa usiku.
Dkt Salma  amesema waathirika wakubwa wa ugonjwa huo ni mama mjamzito na anapoambukizwa ugonjwa wa zika huzaa mtoto mwenye kichwa kidogo na ubongo mdogo na hadi sasa hauna tiba wala tiba ispokuwa mgonjwa hutibiwa dalili za maradhi yanayomsumbua.
Hata hivyo amefahamisha kuwa watoto wenye vidogo waliozaliwa Zanzibar hawakusababishwa na ugonjwa wa zika kutokana na uchaguzi walioufanya.
Mkuu huyo wa  Kitengo cha ufuatiliaji nyendo za maradhi ameeleza kuwa kitengo chake kupitia wizara ya afya imeimarisha huduma za maabara ili kuchunguza ugonjwa wa zia kwa hatua za awali.
Amesema mbu huyo anaweza kuambukiza mwanamke moja kwa moja au kupitia kwa mwanamme aliyeambukizwa kupitia tendo la ndoa.
“ Utafiti umethibitisha kwamba mwanamke anaweza kuambukizwa ugonjwa wa zika kupitia kwa mwanamme mwenye ugonjwa wa zika anaweza kuambukizwa mkewe kupitia damu kwa kufanya tendo la ndoa” amesema Dkt Salma.
Amefahamisha kuwa kirusi cha zika kinaweza kugundulika kuanzia siku moja hadi saba na baada ya hapo mgonjwa anaweza kupata matatizo ya ubongo na miguu kupooza na wajawazito hujifungua watoto wenye vichwa vidogo.
Amesema kitengo hicho kitaendelea kutoa elimu kwa wagonjwa wanaofika hospitali na vituo  vya afya ili kuchukua hatua za kujikinga na ugonjwa huo pamoja na kuwapima wageni wanaoingia nchini kupitia uwanja wa ndege na bandarini.

Kuhusu dalili za ugonjwa huo Dkt Salma amesema amesema ni pamoja na kuumwa na kichwa, maumivu ya viungo, macho kuwa mekundu na kupata vipele vidogovidodo kama harara.

0 comments:

Post a Comment