February 17, 2016

Afisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Zanzibar inakusudia kufanya utafiti wa mwaka wa kilimo na mifugo kuangalia  kiwango cha uzalishaji na mapato yatokanayo na sekta hizo Zanzibar.
Mtakwimu mkuu wa serikali Mayasa Mahfoudh amesema utafiti huo ni miongoni mwa mkakati wa kimataifa katika  kuimarisha takwimu za kilimo na taarifa zitakazopatikana pia zitaisaidia serikali kupata takwimu zitakazotumika kuandaa sera na mipango mbali mbali ya maendeleo ya nchi.
Akizungumza katika mafunzo ya wadadisi watakaofanya utafiti huo amesema uekelezaji wa kazi watashirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya kilimo na Mali asili Zanzibar
Akifungua mafunzo hayo ya siku tano Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Mali asili Affan Othman Maalim amewataka wadadisi hao kuhakikisha wanapata takwimu sahihi na zinazoaminika zitakazosaidia kufahamu ongezeko la kiwango cha mchango wa pato la taifa kwa  sekta hizo.

Utafiti huo unategemewa kuanza Febuari 22 mwaka huu na kuchukua siku ishirini ambapo kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2014 sekta ya kilimo inachangia asilimia 27 ya pato la nchi. 

0 comments:

Post a Comment