February 17, 2016

Wizara ya Afya Zanzibar  imesema vifo vya mama wajawazito vimepunguwa kutoka 337  hadi  286 kwa kinamama laki moja na watoto wanaokufa imefikia 29 kati ya elfu kumi wanaozaliwa hadi disemba mwaka 2014.
Mkurugenzi na Elimu ya Afya Zanzibar Dkt Mohamed Dahoma amesema bado juhudi zaidi zinahitajika kuweza kufikia  lengo la kupunguaza vifo hivyo kwani vile bado kuna changamoto ya katika jamii na utoaji wa huduma za afya ya uzazi Zanzibar.
Amezitaja changamoto hizo ningi zinatokana na maamuzi ya familia na wazee kwa ujumla ikiwemo kutofatilia taratibu za uzazi salama, kutopanga muda wa matayarisho ya  kujifunga na tatizo la usafiri ukifika muda wa mjamzito kujifungua.
Akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto Dkt Dahoma amefahamisha kuwa mradi huo wanalenga unalenga kukabiliana na changamoto hizo kwa kuimarisha utoaji wa huduma stahiki za afya kwa karibu zaidi.
Amesema mradi huo wa miaka miwili  unaojulikana Afya bora ya Mama na Mtoto kwa maendeleo endelevu utawafikia wajawazito elfu 45 na watoto elfu 75 katika shehia 286 za Zanzibar unagharimu zaidi ya shilingi bilioni 23 ikiwa ni  ufadhili wa Serikali ya Canada na unaratibiwa na shirika la kimataifa la Save the children.
Kazi kuu za mradi huu ni kusimamia mama wajawazito kufuatilia huduma za afya, kujitayarisha katika kipindi cha kujifungua na ufuatiliaji watoto hadi katika wiki ishirini na tatu za kuzaliwa kwa vile utaishirikisha jamii katika kusimamia huduma hizo za wazazi.
Akizindua mpango huo ulioenda sambamba na mafunzo kwa watendaji wa afya ya uzazi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Halim Ali Maulid amewataka watendaji wa sekta hiyo kuacha kufanya kazi kisiasa kwani kunachangia kukwamisha kufika malengo ya utoaji wa huduma kwa jamii na utekelezaji wa malengo ya miradi kadhaa inayoanzishwa katika sekta hiyo.
Amesema ni vyema kubadilika kwa vile sekta ya afya sasa inalaumiwa kwa kuwa na utendaji mbaya wa kazi usiofuata maadili hivyo ni vyema kubadilika kwani wao hawako katika kuchezea maisha ya watu.
“Acheni kucheza na maisha ya watu kama huwezi kufanya kazi acha na kama siasa basi nenda huko si kuingiza masuala hayo katika kazi haipendezi”. amesema Naibu Halima.
Amesema kuanzishwa kwa mradi huo ni hatua muhimu ya kuweza kufikia malengo ya serikali ya kupunguza vifo hivyo vya mama wajawazito na watoto ambavyo vingi vyanzo vyake vinavyotokana na uzembe vinaweza kuzuilika iwapo kutatolewa huduma bora na elimu kwa jamii, familia, wazee na wanandoa wenyewe.
Halima amefahamisha kuwa kufanikiwa hilo mradi huo utafikia lengo na kuwa mfano katika utekelezaji wake hali inayoweza kuongeza ushawishi kwa wafadhili kuendelea kusaidia masuala ya uzazi n malezi salama ya mototo Zanzibar.





Meneja mradi wa Afya bora ya Mama na Mtoto kwa  maendeleo 
endelevu Zanzibar kutoka Save the childrens Dkt Bernard mbwele 
akitoa  mada juu ya mradi huo 


0 comments:

Post a Comment