January 02, 2016

Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema uchaguzi wa marudio upo na bajeti yake imeshatengwa na wanachosubiri ni mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Zanzibar atangaze tarehe ya kufanya uchaguzi huo.
Amesema bajeti hiyo haitatofautiana na ile iliyotumika katika uchaguzi wa Novemba 2015 iliyofikia karibu ya shilingi bilioni saba.
Amekanusha kauli kuwa uchaguzi huo hautafanyika kwa vile matokeo yanayolazimisha kutangazwa na CUF yameshafutwa kwa mujibu wa sheria kutokana na kasoro kadhaa zilizojitokeza.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya miaka 52 ya mapinduzi Balozi Seif amesema mazungumzo yanayoendelea ni ya kuhakiksha amani inaimarika Zanzibar na si suala la uchaguzi uliofutwa.
Akizungumzia kuhusu maadhimisho ya miaka 52 sherehe za Mapinduzi Balozi Seif amewabeza wanaosusuia sherehe hizo kwa madai kuwa Rais Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein kuwa si halali ni upotoshwaji mkubwa.
Amefahamisha kuwa rais yupo kihalali na hata mawaziri wake wote na watamaliza ukomo wao hadi atakapoapishwa rais mwengine kama ilivyoanishwa   katika katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na si kama inavyeleezewa kuwa ukomo wake umeisha tangu tarehe 2 Novemba.
Kwa mujibu wa Balozi Seif maadhimsiho ya sherehe hizo yanayotarajiwa kuanza kesho Jumapili 3 January 2016 kwa shughuli za usafi na ufunguzi wa miardi ya maendeleo 24 zitafikia kilele chake Januari 12 katika uwanja wa Aman. 




0 comments:

Post a Comment