Serikali imepoteza jumla ya Shilingi
bilioni 48.47 baada ya makontena 11,884 na magari 2,019 kupitishwa
badarini Dar es Salaam bila kulipiwa kodi.
Kufuatia kashfa hiyo watu 7 wanashikiliwa na
wengine 8 wanatafutwa na Jeshi la Polisi kwa kuhusishwa na ukwepaji kodi huo
uliolikosesha taifa mapato.
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es
Salaam, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa
Makame Mbarawa amesema ufisadi huo umebainika
baada ya serikali kuzifanyia ukaguzi bandari zote za nchi kavu (ICDs) jijini
Dar es Salaam.
Akifafanua Waziri
Mbarawa amesema makontena hayo 11,884 yalikuwa na thamani ya Sh 47.4 bilioni
wakati magari gari 2019 zenye thamani ya sh 1.07bilioni yalitolewa bandarini
pasipo kulipiwa.
0 comments:
Post a Comment