Shirika la biashara la taifa la Zanzibar ZSTC limefanikiwa
kununua tani 1730 za karafuu zenye
thamani ya shilingi bilioni 24.2.
Karafuu hizo zimenunuliwa kuanzia Julai 9 hadi Disemba 18
mwaka huu kwa wakulima mblimabli wanaozlisha zao hilo.
Mkurugenzi wa ZSTC mwanahija almasi ali amekanusha madai kuwa shirika hilo
halina fedha za kununulia karafuu na badala yake linatoa risiti za
malipo kwa wakulima si ya kweli.
Amefahamisha kuwa ZSTC ina fedha za kutosha za kununulia
karafuu katika kipindi chote cha manunuzi na hakuna mu atakae kopwa fedha
zake.
Kuhusu kuweka alama zao
hilo (BRANDING) amesema taratibu za
mpango huo zimeshakamilika na wakati wowote inaweza kutumika.
0 comments:
Post a Comment