Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzani Dkt. John Pombe Magufuli amewaapisha Mawaziri aliowateuwa hivi
karibuni kukamilisha baraza lake la mawaziri.
Katika hafla hiyo iliyofanyika Ikulu
jijini Dar-es-salaam waliapishwa ni Prof Jumanne Abdalah Magembe Waziri wa Maliasili
na Utalii, Dkt Joyce Ndalichako Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi,
na Waziri wa Fedha Mipango Dkt Philip Isdori Mpango.
Wengineo ni waziri wa maji na umwagiliaji Mhandisi
Gerson lwenge, Prof Makame Mnyaa
Mbarawa Waziri wa ujenzi uchukuzi na Mawasiliano na Hamad Masauni Yusuph Naibu Waziri
wa Mambo ya ndani ya nchi.
Mawaziri hao baada ya
kuapishwa wameeleza kuwa watafanya kazi sambamba na kasi na kauli mbiu ya hapa
kazi tu kwa kuzingatia wizara watakazoziongoza kuwa ni nyeti na za msingi kwa
uchumu na maendeleo ya Tanzania.
Baadhi ya mawaziri hao waliwasili wizarani
mwao muda mfupi baada ya kuapishwa na kufanya vikao na viongozi na watendaji ili
kujitambulisha.
0 comments:
Post a Comment