Hali
mbaya na ukataji wa miti kiholela kwa ajili ya kupata maeneo ya ujenzi
umekithiri kwa kiwango kikubwa na kutishia usalama wa mazingira ya visiwa vya Zanzibar.
Miti
iliyoathirika zaidi ni minazi na inakisiwa zaidi ya milioni 4 imekatwa maeneo mbalimbali
ya mkoa wa mjini magharibi katika ardhi
za mshamba walizopatiwa wananchi na serikali kuyaendeleza.
Mkurugenzi
wa idara ya misitu na maliasili zisizorejesheka Zanzibar Sheha Idrissa Hamdan
amesema wilaya ya magharibi A na B ndio zilizoathirika zaidi kutokana na kasi
kubwa ya ujenzi wa makaazi na watu
wanajenga bila ya kufuata taratibu zilizowekwa serikali.
“
Tumebaini minazi milioni 9 kati ya milioni 13 imeshakatwa katika kipindi cha miaka
10 watu wanajiamulia tu pasi na kuwaarifu idara inayoshughulika na ardhi
halmashauri ” amefahamisha.
Ameeleza
kwa suala hilo halikubaliki kufumbiwa
macho hatua za lazima zinapaswa kuchukuliwa ili kunusuru zao hilo lisipotee
kabisa.
Mkurugenzi
Hamdani amefahamisha kuwa athari za ukataji wa minazi kiholela zimeshaanza kuonekana
ikiwemo Zanzibar kuanza kutegemea nazi kwa ajili ya matumizi kutoka Tanzania
bara wakati ilikuwa miongoni mwa vinara wa kusafirisha zao hilo pamoja na mafuta na mbata nje ya
nchi.
Akizungumzia
juhudi wanazochukuwa amesema wamepitisha sheria namba 10 ya kulinda misitu na
hivi karibuni Serikali imetoa sheria mpya ya kudhibiti msumeno wa moto na Disemba
7 2015 ilikuwa tarehe ya mwisho ya watu wanayoimiliki kuirejesha lakini
inaendelea kutumika kwa siri kukata miti.
Hamdani
amesisitiza kuendelea kuelimisha na kuhamasisha utunzaji wa misitu kwa vile
bado wapo wahalifu wachache wanakiuka hayo ili kuhakikisha matumizi ya
rasilimali yanaendana na utaratibu uliowekwa.
Hata hivyo amesema zanzibar haijachelewa kuchukuwa hatau hizo lakini ni vyema kuwepo na ushirikiano
kati ya taasisi mbalibali zikiwemo za wilaya,
halamashauri na vyombo vya ulinzi ili asilimia 40 ya eneo la Zanzibar lenye msitu kuendelea kudumu kwa faida ya nchi.
0 comments:
Post a Comment