December 10, 2015


Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kutunza na kulinda Utamaduni wa Zanzibar na kuyafanyia matengenezo  majengo ya Mji  Mkongwe yaliyochoka kwa ushirikiano wa Mfuko wa Kimataifa wa kuyaendeleza majengo  ya  Miji Mikongwe Duniani na kuyatunza {World Monument Fund}.
Hayo yamesemwa  na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni,Utali na Michezo Issa Mlingoti wakati akifungua mkutano kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo  wa kutembelea na kuzungumzia namna ya kuyafanyia matengenezo majumba  mabovu ili yasitoweke katika Mji huo.
Amese matengenezo hayo  hufanywa kwa mashirikiano ya pamoja kati ya Serikali, wahisani na Mashirika mbalimbali  ya Kimataifa.
 Nae Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Mji Mkongwe Zanzibar  Issa Makarani amesema  hivi sasa kuna majengo yapo hatarini kupotea katika urithi wa Kimataifa  kutokana na kuchakaa na  kufikia hatua ya  kuanguka hivyo kutokea mfuko huo kusaidia ni jambo la faraja.
 Aidha alisema  wananchi  kwa upande wao wanalazimika kufuata kanuni na taratibu za  kuuhifadhi na kuulinda Mji Mkongwe wa Zanzibar ikiwamo kuacha kupitisha magari makubwa ambayo hupelekea kupasuka kwa majengo.
“Kuazia mwakani kutakua na sheria maalumu ya kupitisha vyombo vya moto katika maeneo ya Mji Mkongwe wa Zanzibar ambayo madereva watalazimika kuifuata,” alisema Makarani.
Nae Meneja wa  Mfuko wa Kimataifa wa kuyaendeleza majengo  ya  Miji Mikongwe Duniani na kuyatunza kwa nchi za  Jangwa la Sahara Stephen Battle  amesema taasisi hiyo imekuwa ikifanya matengenezo majengo ya miji yenye urithi wa Kimataifa ikiwemo Kanisa la Mkunazini liliopo Mji mkongwe wa Zanzibar.



0 comments:

Post a Comment