Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi
amemuagiza Mmiliki wa Kiwanja kinachotaka kujengwa Nyumba ya Ghorofa katika
Mtaa wa Mlandege Anuari Abdulla kusitisha
mara moja ujenzi huo.
Hatua hiyo imekuja kufuatia malalamiko makubwa yaliyotolewa
na wakaazi wa Mtaa huo wakimshutumu Mmiliki huyo kuvamia eneo la wazi katika
sehemu hiyo.
Balozi Seif alimuonya Mmiliki huyo iwapo ataendelea kukaidi
agizo alilopewa na taasisi zinazosimamia na kushughulikia masuala ya
Ujenzi Serikali italazimika kumchulia hatua za kisheria dhidi yake.
“ Tumebaini unaendelea kwenda kinyume na maamuzi uliyopewa
ya kusitisha ujenzi wa Jengo lako sasa iwapo utaendelea kufanya hivyo Serikali
italazimika kukuchukulia hatua za kisheria zinazofaa “. amesema Balozi Seif.
Amefahamisha kuwa wakaazi wa Mtaa wa Mlandege kuzingatia matakwa
yaliyokubalika katika uhifadhi wa eneo la Mji Mkongwe lililopata hadhi ya kuwa
Urithi wa Kimataifa ambapo mtaa huo pia umo ndani ya mji huo wa Kihistoria.
Mapema Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uhifadhi na Uendelezaji
Mji Mkongwe wa Zanzibar Issa Sarboko Makarani ameeleza kuwa Mmiliki wa
kiwanja hicho amekuwa akikaidi maamuzi anayopewa kuyatekeleza na mamlaka husika
katika ujenzi huo.
“ Kibali cha Ujenzi wa Jengo hili kinachodaiwa kutolewa na
Baraza la Manispaa Zanzibar kimefutwa kwa pamoja na wakurugenzi Wanne wa Idara
za Ardhi, Mamlaka ya Mji Mkongwe, Baraza la Manispaa pamoja na Idara ya Ujenzi
na Mipango Miji “. amefafanua Sarboko.
Amesema Anuari ameamua kuendeleza ujenzi huo kwa kutumia
kibali kilichofutwa alichopewa na Mmoja
wa Afisa wa Baraza la Manispaa kwa vile hakikuzingatia sheria na taratibu
zilizowekwa.
0 comments:
Post a Comment