Jeshi la polisi Mkoa wa kusini Pemba limetakiwa kuzisimamia
kikamilifu kesi 27 zilizobakia za makosa ya udhalilishaji zilizopo mahakamani
ili kupatia hukumu kwa mujibu wa sheria.
Amesema ni jambo la kusikitisha kwa kesi 64 za udhalilishaji
zilizoripotiwa katika kituo cha mkono kwa mkono Disemba 2014 hadi mwezi huu wa Disemba
2015 kesi 13 tu zimehukumiwa na kesi 27
zikiendelea mahakamani huku kesi 24 zimeshafutwa mahakamani.
kauli hiyo ameitolewa na Mkuu wa wilaya ya Chake Chake Hanuna Ibrahim
Masoud amelitaka katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia
dhidi ya wanawake na watoto.
Kamanda wa polisi Mkoa wa kusini Pemba Mohamed Sheikhan Mohamed
ameahidi kuzisimamia kesi hizo kupatiwa hukumu sambamba na kuvikomesha vitendo
hivyo.
Hata hivyo amesema ili lengo la kudhibiti vitendo vya udhalilishaji
wa wanawake na watoto liweze kufanikiwa lazima kuwe na nguvu ya pamoja kati ya jeshi
hilo, afisi ya Mkugenzi wa mashtaka, Mahakama na wananchi.
mapema mwenyekiti wa mtandao wa polisi wanawake walioandaa
maadhimisho hayo Asha Tahir Silima amesema mtandao huo unaendelea kutoa elimu
katika ngazi mbali mbali kuhusu makosa ya udhalilishaji pamoja na kuimarisha
huduma za dawati.
0 comments:
Post a Comment