Leo
Rais John Magufuli ameongoza Watanzania kutumia Siku ya Uhuru kufanya usafi,
yuko eneo la ufukwe karibia na Ikulu akifanya usafi.
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa naye alikuwa kwenye soko la Kariakoo akiongoza
wafanyabiashara wa soko hilo kufanya usafi.
Ni
siku ya kihistoria kwa taifa tofauti na ilivyokuwa imezoeleka kwamba siku ya
maadhimisho ya Uhuru watu huelekea viwanja vya Uhuru kuungana na wengine
kuadhimisha siku hii ambapo leo ni miaka 54 tangu uhuru kupatikana,lakini
watu wanafanya usafi kuboresha mazingira ikielezwa ni UHURU na KAZI, ikienda
sambamba na kaulimbiu ya Hapa Kazi Tu.
0 comments:
Post a Comment