Wizara ya Fedha na
Benki ya Maendeleo Afrika(ADB) zimesaini mikataba yakuikopesha Tanzania
shilingi bilioni 750 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi sekta mbili za
maendeleo ya ujenzi wa barabara na viwanja vya ndege nchini.
Mikataba hiyo imesainiwa leo jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu
wa Wizara ya Fedha Dkt Servacius Likwelile kwa upande wa Tanzania na Mwakilishi
wa Benki hiyo Dkt Tonia Kandiero.
Akizungumza mara baada ya kusaini mikataba hiyo Dkt . Likwelile
alisema kuwa katika mkopo wa kwanza utasaidia katika kuinua uchumi nchini kwa
kuimarisha miundo mbinu ya barabara ya Tanzania bara na visiwani.
Dkt Servacius Likwelile aliongeza kuwa,mradi huu utapunguza gharama za matengenezo ya barabara pamoja na muda usafirishaji na ukarabati wa vyombo vya usafirishaji.
Dkt Servacius Likwelile aliongeza kuwa,mradi huu utapunguza gharama za matengenezo ya barabara pamoja na muda usafirishaji na ukarabati wa vyombo vya usafirishaji.
Naye Mwakilishi wa Benki Maendeleo ya Afrika Dkt Tonia Kandiero
alisema kuwa fedha hizo zitasaidia kuimarisha miundo mbinu ya barabara kwa
ajili ya kuimarisha kilimo hasa katika mikoa ya Tabora, Katavi na Ruvuma ambapo
asilimia 90 ya watu wake ni wakulima.
Maeneo ambayo mradi huu yatakayoshughulika ni barabara ya kutoka Tabora (Pangale) hadi Mpanda na nyingine kutoka Mbinga hadi Mbamba Bay kwa Tanzania Bara na kwa Zanzibar barabara itatoka Bububu hadi Mkokotoni na nyingine kutoka vijijini hadi Bitumen standadi.
Mkopo mwingine unaelekezwa katika ujenzi wa viwanja vya ndege vya Msalato kwa Tanzania Bara na Pemba kwa Zanzibar.
Maeneo ambayo mradi huu yatakayoshughulika ni barabara ya kutoka Tabora (Pangale) hadi Mpanda na nyingine kutoka Mbinga hadi Mbamba Bay kwa Tanzania Bara na kwa Zanzibar barabara itatoka Bububu hadi Mkokotoni na nyingine kutoka vijijini hadi Bitumen standadi.
Mkopo mwingine unaelekezwa katika ujenzi wa viwanja vya ndege vya Msalato kwa Tanzania Bara na Pemba kwa Zanzibar.
Jacquline
Mrisho-maelezo Dsm
0 comments:
Post a Comment