November 28, 2015


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto Msham Abdalla Khamis amewashauri watendaji wa vyombo vya sheria  kutatua changamoto zinazokwamisha kesi za ukatili na udhalilishaji wa kijinsia ili kuwatia hatiani watuhumiwa wa vtendo hivyo  kwa mujibu wa sheria.

 Amesema bado tatizo hilo ni kubwa na taifa linapata hasara kubwa ya kuharibiwa watoto ambao ni rasilimali ya taifa na wengi wao huathirika kisaikolojia na kupata matatizo makubwa ya kiakili.
Akifungua warsha ya kuwajengea uwezo wadau hao wa kushughulikia kesi za ukatili na udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar amesema kutochukuliwa hatua za kisheria kwa wakati muafaka kunawafanya watuhumiwa  wa makosa hayo kujenga kiburi na kusabisha  kuongezeka kwa makosa hayo.
Nao watendaji hao wa vyombo vya sheria Zanzibar wamesema yapo matatizo mengi yanayosababisha kesi nyingi za aina hiyo kukwama kusikilizwa ama kumalizwa kinyeji , ikiwemo kutokufika mashahidi muhimu Mahakamani au watu kusameheyana.
Wamesema kazi inayotakiwa kutiliwa mkazo ni kutoa elimu kwa jamii na ili wawe tayari kutoa ushahidi mahakamani utakao mtia hatiani mtuhumiwa na kupewa adhabu kubwa inayomstahikia.
Mafunzo hayo yametayarishwa na Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto na kuwashirikisha watendaji mbali mbali wa vyombo vya sheria ikiwemo Polisi katika madawati ya kijinsia, Mahakimu, Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka na watendaji wengine wa Wilaya na Mkioa wa Wizara hiyo.

0 comments:

Post a Comment