Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
ameamuru fedha zilizopaswa kutumika kugharamia shamra shamra za siku ya Uhuru za
tarehe 09 Desemba 2015, kutumika kufanya upanuzi wa barabara ya Mwenge hadi
Morocco jijini Dar es Salaam yenye urefu wa kilometa 4.3 kwa kuongeza njia
mbili za barabara za lami.
Tayari fedha hizo kiasi cha shilingi bilioni nne zimepelekwa kwa
wakala wa barabara Tanzania TANROADS kwa
ajili ya utekelezaji wa agizo hilo, linalopaswa kuanza mara moja.
Kujengwa kwa njia hizo kutaifanya barabara ya Morroco hadi
Mwenge kuwa na njia tano.
0 comments:
Post a Comment