Jeshi
la Polisi linawashikilia watu 12 kwa tuhumiwa wa upotevu wa makontena 349
katika bandari ya Dar es Salaam .
Watu
hao miongoni mwao ni waliotajwa na Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa na
wengine wamebainika kufuatia uchunguzi unaoendelea.
Akitangaza
baadhi ya majina hayo Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai Diwani
Athumani amesema baadhi ya majina hayatawekwa hadharani hadi upelelezi utakapo
kamilika ili kupeleka watuhumia wote mahakamani.
Akiongea
na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa
ya Jinai amesema uchunguzi unaofanywa na wataalamu waliobobea wa makosa ya uhalifu wa kifedha umeweza
kuwabaini watu hao wamehusika na wizi huo.
Kamanda
Athumani amesema kati ya watuhumiwa hao kumi na mbili watano wanashikiliwa na
Jeshi la Polisi na saba bado upepelezi unaendelea na utakapokamilika
watafikishwa mahakamani.
Wanaoshikiliwa
kutokana na tuhuma mbalimbali ni Kamishna wa Idara ya Forodha na Ushuru TRA
Tiagi Masamaki, Meneja Kitengo cha Huduma za Ushuru na Habib Mponezia,
Msimamizi Mkuu wa Kitengo cha Ushuru wa Forodha.
0 comments:
Post a Comment