Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
amehudhuria hafla fupi iliyoandaliwa kwa ajili ya wabunge katika viwanja vya
Bunge Mjini Dodoma na kuagiza fedha zilizochangwa kwa ajili ya kugharamia hafla
hiyo zipelekwe Katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kununulia
vitanda vya wagonjwa.
Mheshimiwa Magufuli ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa
kuwa wadau mbalimbali wamechanga kiasi cha shilingi milioni 225 kwa ajili ya
kugharamia hafla ya wabunge katika siku ya uzinduzi wa Bunge.
Dkt Magufuli amesema alipata taarifa za kuwepo kwa michango hiyo
ya fedha na kutoa maelekezo hayo ili zikatumike kupunguza tatizo la wagongwa
wanaolala chini kutokana na uhaba wa vitanda unaikabili hospitali hiyo.
“kwa kufanya hivyo tutakua tumejinyima sisi wenyewe lakini tutawanufaisha
wenzetu wenye matatizo makubwa yanayoweza kutatuliwa kwa fedha hizo”.
Awali akitoa taarifa ya michango hiyo Ofisa wa Spika wa
Bunge Said Yakubu amesema kati ya shilingi milioni 225 zilizochangwa ni
shilingi milioni 24 tu ndio zilizotumika katika hafla hiyo baada ya kuzingatia
maagiza ya Rais Magufuli.
Rais Magufuli amekabidhi vyeti vya kutambua mchango wa wadau
waliochangia fedha wakiwemo Benki za NMB, CRDB na Benki ya Afrika pamoja na
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PSPF na PPF.
0 comments:
Post a Comment