November 20, 2015

Rais wa Jamuhuri Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli amelihutubia bunge kwa mara ya kwanza huku akiwataka watanzania kuwa serikali yake itatenda haki kwa kila mtanzania.

Amesema pia haitafumbia macho wale wenye nia mbaya ya kuvuruga amani kwa kuwa serikali inalengo la kuwatumikia wananchi ili kuindokana na ukata wa umasikini.

Ametaja vipaumbele vya serikali yake ni pamoja na kupunguza urasimu kubana matumizi serikali, kurejesha nidahmu ya serikali na uwajibikaji kwa watumishi wa umma na viongozi kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.

Dk.Magufuli ameapa kuwashugulikia wala rushwa na mafisadi bila kuwaonea haya ya aina yoyote kwani ndio wanaorudisha nyuma maendeleo ya taifa kwa kutumia raslimali ya watanzania vibaya na kuomba bunge,Takukuru na wananchi wenyewe kumuunga mkono.
“Nasema hili kwa kuwa anadhanira ya kweli ya kuifanya Tanzania iwe nchi ya kipato cha kati”Dk.Magufuli amesema.
Ameeleza kuwa kiu yake ni kuhakikisha uchumi wa kipato cha kati unafanana na maisha ya wananchi wa Tanzania ili wafurahie matunda ya taifa lao kwa kuimarisha sekta ya viwanda.
Katika kukahikisha hilo amewataka waliobinafsisha viwanda kuhakikisha kuwa wanawajibishwe kwani alishawahi  kusema nia yake ni kuimarisha viwanda ili watu wafurahie soko la ndani na kuzalisha ajira nyingi ifikapo 2020.
Akizungumzia kuhusu sekta ya elimu Dk.Magufuli amesema utoaji wa elimu bure kuanzia elimu ya msingi hadi sekondari ni wenye dhamira ya kweli kwa serikali yake.
Pia ameahidi kuwa wanafunzi wa elimu ya juu chini ya serikali watapewa mikopo kwa wakati unaostahili.
Kuhusu Muungano Zanzibar na Tanganyika Dk.Magufuli amesema ataushughulikia na kuulinda kwa vile nchi hizo zimeungana zikiwa nchi huru.
Katika hotuba yake Rais Magufuli amelaani vikali kitendo cha Wabunge wa Vyama vya Upinzani kuzomea viongozi wa Serikali bungeni na kuwaeleza kuwa hawajakomaa kisiasa na kuwaita watoto.
Mmeona tuna kazi kubwa, bado tuna watoto wengi. Tuendelee kuwavumilia, nadhani na watanzania wameona…… Ndio maana nimekupongeza sana Mheshimiwa Zitto umekomaa na naamini” amesema rais Magufuli.
Hata hivyo amewataka wabunge wote kusimama pamoja bila kujali itikadi zao za vyama na kuacha masuala ya kupigana vijembe, kuzomeana na kutoka nje.

0 comments:

Post a Comment