Chama cha mapinduzi CCM Zanzibar kimekanusha taarifa
zilisambazwa katika mitandao ya kijamii zinazohusiana kuwa chama hicho
kimeridhia kuapishwa kwa maalim Seif kuwa rais wa Zanzibar.
Naibu katibu mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai amesema kauli hizo hazina ukweli
na ni mpango maalum wenye nia ya kuvuruga amani ya nchi .
Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi kuu ya CCM Kisiwandui mijini Zanzibar amesema lengo la
taarifa hizo ni wanaccm na wapenda amani wasiweze kuendelea na shughuli zao za
kujiletea maendeleo.
0 comments:
Post a Comment