Mahakama ya rufaa ya Tanzania imeanza kazi ya kusikiliza mashauri
21 ya kesi za rufaa upande wa Zanzibar na kutolewa uamuzi.
Mashauri hayo yatasikilizwa katika mahakama kuu ya Zanzibar ni
pamoja na kesi za madai na jinai.
Akitoa ufanunuzi jaji Mkuu wa Tanzania jaji
Mohammed Chande Othaman juu ya mashauri amesema
watasikiliza kesi hizo kuanzia sasa hadi Disemba 14.
amesema kati ya mashauri hayo yatakayosikilizwa mengi ni
ya madai na matatu yatakuwa ya kesi za jinai.
Jaji Chande amefahamisha kuwa mashauri hayo ni
wadai na wadaiwa na wamekuwa na mawakili wa kuwakilisha katika
kesi ikiwa ni utaratibu uliyowekwa katika
mahakama ya rufaa.
Ameeleza kuwa mahakama ya rufaa itahakikisha kila
mmoja anapata fursa ya kutumia haki yake kwa mujibu wa sheria.
Kikao hicho cha kwanza cha mahakama ya rufaa kilitanguliwa na
ufunguzi wa gwaride kuashiria kuanza kwa vikao.
0 comments:
Post a Comment