November 30, 2015


Mahakama ya hakimu mkazi Morogoro imemuachia huru Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda aliyekuwa akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi baada ya upande wa mashtaka wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka yaliyofunguliwa mahakamani hapo dhidi yake.

Sheikh ponda alikuwa anakabiliwa na makosa mawili ikiwemo kushawishi watu kutenda kosa, pamoja na kutoa matamshi yanayoumiza imani ya dini nyingine amekaa rumandae kwa zaidi ya miaka miwili kutokana na kuzuiliwa dhamana yake kwa maslahi ya taifa.
Hakimu wa kesi hiyo Mary Moyo amesema ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka haukujitosheleza hivyo mahakama hiyo imemwachia huru na rufaa iko wazi endapo upande wa mashitaka hautaridhika.
Akizungumza baada ya kuachiliwa huru sheikh ponda ameishukuru mahakama kwa kutenda hakijapo kuwa imechelewa kutoa hukumu.

0 comments:

Post a Comment